KARIBU

tujifunze pamoja jinsi ya kufanya mambo mbalimbali; +255 758100222, tuma maoni, omba mada, dhamini mtando n.k jinsiya.tz@gmail.com

Wednesday, 15 January 2014

JINSI YA KUPANGILIA PICHA, KUPENDEZESHA PROFILE ZA FACEBOOK



Picha ndo radha halisi ya  Facebook. Bila ma picha picha hautaona kitu bali mahabari ya siasa, mara nani kafanya nini au maelezo yasiyotuhusu, hakuna anaeingia facebook kusoma novel, hadithi au habari zisizomhusu bhana! Ila picha! Picha zina amsha amsha facebook – la hasha hatuna mbaya na jamaa yako anaepost habari flani zisizotuhusu kila saa.

Ingawa hata ukitupia picha facebook bila mpangilio bado utawavutia marafiki zako, lakini mbona bado sio kazi, chukua muda wako mchache tu kupangilia maingizo ya picha zako ili kuvutia marafiki zako zaidi na zaid.
Kuna njia kama tatu hivi za msingi kufikiria katika kuedit picha za facebook.
 Moja; ni katika uchaguzi wa picha gani iingie kwenye ukurasa yako wa facebook, ya pili ni kutumia software / programu maalum za kuboreshea picha na ya tatu I kuweka mpangilio ambao utavuta na kua bora kutazamwa na marafiki wa kila aina.
Tuanze na kipengele cha kwanza – kuchagua aina za picha za kutupia facebook. Hiki ni kipengele rahisi zaidi. Kwanza usiweke picha yoyote ambayo unafikiri wewe mwenyewe usingependa kuiona au watu flani hawata penda kuona.kua mwangalifu juu ya aina ya picha unazotaka kushare na usijidhalilishe wewe au marafiki zako; vinginevyo utapoteza baadhi ya marafiki.usiboe watu kwa kutupia picha hamsini za mbwa wenu mbaya mmoja akijisaidia. Usiweke picha za ngono.
Na tukija kwenye suala la ku edit picha zenyewe, una mambo kadha wa kadha ya kuchagua;
Ø  Kuna programu nyingi za bure mtandaoni unazoweza kutumia  kama utakavyojifunza kwenye makala zinazokuja.
Ø   Kama bajeti inaruhusu wape kazi wataalamu wa kuedit picha, sio mbaya.
Mwisho, mtandao wa facebook unakupa njia kadhaa za kupangilia picha zako, kwa mfano unaweza kuweka picha katika albam tofauti tofauti. Kurahisisha upatikanaji wa picha zako, zipange kwa matukio, kwa mfano. Mkesha wa krismasi, mwaka mpya au serengeti tour.

Ungependa kuchangia mawazo zaidi? Tafadhali tuandikie> jinsiya.tz@gmail.com

No comments:

Post a Comment